Page:Swahili tales.djvu/470

This page has been proofread.
450
HADITHI YA LIONGO.

mbie, na akiisha kufa tutakupa ufaume. Akawajibu, vema.

Akaenda. Alipofika akamkaribisha, akamwambia, umekuja fanya nini? Akamwambia, nimekuja kukutazama. Akamwambia, najua mimi umekuja kuniua, na hao wamekudanganya.

Akamwuliza, baba, kitu gani kinachokuua? Akamwambia, sindano ya shaba, mtu akinichoma ya kitovu, hufa.

Akaenda zake mjini, akawajibu, akawaambia, sindano ya shaba ndio itakayo'mua. Wakampa siudano, akarudi hatta kwa babaye. Alipomwona, akaimba yule babaye, akamwambia—

Mimi muyi ndimi mwe mao, situe
Si mbwenge mimi muyi ndimi mwe mao.

Maana yake, Mimi mbaya ndiye mwema wako, si nifanya mbaya, mimi ndimi mbaya ndiye mwema wako. Akamkaribisha, akajua, huyu amekuja kuniua.

Akakaa siku mbili, hatta siku hiyo usiku amelala, akamchoma sindano ya kitovu. Akaamka kwa uchungu wake, alishika uta wake na viembe, akaenda hatta karibia visima. Akapiga magote, akajitega na uta wake. Akafa palepale.

Hatta assubui, watu wanaokuja teka maji wakamwona, wakamthani mzima, wakarudi mbio. Wakatoa khabari mjini, leo maji hayapatikani. Kulla endaye hurudi mbio. Wakatoka watu wengi wakaenda, wakifika, walipomwona wasiweze kukaribia, wakarudi. Siku tatu watu wanathii kwa maji, kuyakosa.